Miaka 10 ya HakiElimu

Mgeni rasmi katika sherehe za miaka kumi ya hakiElimu ambaye ni Mh. Samuel Sita

Young Boys Carrying Sand in a Pull Cart After Attending School

Young boys carrying sand in a pull cart after attending school to earn probably stationery money at Midizini area in Manzese

>Mathematicians in the Making....

Samia Tajiri(right)of Kiwalani Primary School in Dar es Salaam does her mathematics homework using bottle caps at a street side

Tuesday, September 18, 2012

Kila la heri darasa la saba kwenye mitihani yenu ya mwisho

 

Wanafunzi wa darasa la saba nchini kote kesho na keshokutwa wanatarajia kuanza mitihani ya kumaliza elimu yao ya msingi ambapo kwa mara ya kwanza tekinolojia mpya iitwayo Optical Mark Reader (OMR) itatumika.
Watahiniwa watatumia fomu maalum za OMR kujibia mtihani na majibu yao yatasahihishwa kwa kutumia kompyuta.  Masomo yatakayotahiniwa katika mtihani huo ni Kiswahili, English Language, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii. 
Jumla ya wanafunzi 894,881 wamesajiliwa  kufanya mtihani huo ambapo wavulana ni 426,285 sawa na asilimia 47.64  na wasichana ni 468,596  sawa na asilimia 52.36. Aidha, kati ya  wanafunzi hao, wapo wanafunzi 874,379  watakaofanya mtihani huo kwa lugha ya Kiswahili na wanafunzi 20,502 watafanya kwa lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo waliyoitumia kujifunzia.  Wanafunzi wasioona waliosajiliwa kufanya mtihani ni 92 wakiwemo wavulana 53 na wasichana 39.  Watahiniwa wenye uono hafifu ambao huhitaji maandishi makubwa ni 495, kati yao wavulana ni 238 na wasichana ni 257.
 
Mwaka jana, watahiniwa 1,010,619 waliandikishwa kufanya mtihani wa darasa la saba mwaka 2011 ambapo jumla ya watahiniwa 993,324 waliandikishwa kufanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili na watahiniwa 17,295 waliandikishwa kufanya mtihani kwa lugha ya  Kingereza ambayo walikuwa wakiitumia katika kujifunzia.



HakiElimu inawaasa wanafunzi, walimu na wadau wote kuzingatia misingi bora katika kipindi chote cha mitihani ya kumaliza elimu ya msingi ikiwa ni daraja moja muhimu linalotakiwa kuwavusha wanafunzi kutoka elimu ya msingi na kuingia elimu ya sekondari.
Kila la heri wanafunzi wote katika mitihani yenu.


Wednesday, August 22, 2012

Mitaala shule za msingi inawachanganya wanafunzi – Walimu

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Kitopeni kutoka Wilaya ya Korogwe.
BAADHI ya walimu wa shule za msingi wilaya za Korogwe na Moshi wamelalamikia mabadiliko ya mara kwa mara ya mitaala kwa shule za msingi pamoja na idadi kubwa ya masomo kwa wanafunzi wa madarasa ya chini, kuwa yamekuwa yakiwachanganya wanafunzi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti hivi karibuni walisema mabadiliko ya mara kwa mara kwa mitaala yanayofanywa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi bila maandalizi yamekuwa chanzo cha vikwazo cha kufanya vizuri kwa sekta hiyo.

Akizungumza hivi karibuni na mwandishi wa habari hizi, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Gerezani, mjini Moshi, Khadija Mtui alisema mabadiliko ya mitaala ya mara kwa mara yanawachanganya wanafunzi pamoja na walimu hivyo kuwa kikwazo.

Alishauri kuwepo na maandalizi ya kutosha ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha walimu ambao ni wadau wakubwa wa sekta ya elimu kabla ya mabadiliko ya mitaala hiyo. Alisema pamoja na hali hiyo mabadiliko ya vitabu vya masomo bila utaratibu mahususi ni tatizo pia katika mafanikio ya sekta hiyo kitaaluma.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Lwengera Darajani, wakiwa wamapumziko
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kitopeni ya Mjini Korogwe, akizungumza na mtandao wa Thehabari.com hivi karibuni.
“Mabadiliko ya mitaala na mchanganyiko wa vitabu bila utaratibu mahususi ni tatizo, kwa sasa hivi kila shule ina kitabu chake katika somo fulani…hata hivyo licha ya mabadiliko ya mara kwa mara hakuna maandalizi, mimi tangu nimalize chuo 1979 sijaenda semina yoyote wala mafunzo kujiandaa na mabadiliko ya mitaala hii. Hili linachangia pia,” alisema mwalimu Mtui.

Akifafanua zaidi Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Muungano, ya wilayani Moshi, Ashati Elihaki alisema mbali na mchanganyiko juu ya suala la vitabu vya masomo mabadiliko ya mitaala yamegeuza baadhi ya masomo kubaki kama ‘kiini macho’ jambo ambalo ni tatizo kwa walimu.

“…angalia kwa mfano somo kama la Tehama linaloanza kufundishwa darasa la tatu hadi la saba somo hili lipo kinadharia zaidi, hakuna walimu ambao wameandaliwa kufundisha somo hili lakini linatakiwa kufundishwa eti kwa kutumia mwongozo wa mwalimu kimsingi hii si sawa,” alisema Elihaki.
Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kitopeni ya Mjini Korogwe, Theodolph Karigita alisema tofauti na ilivyokuwa hapo awali mitaala ya sasa imevurugwa kiasi kikubwa jambo ambalo linawachanganya walimu na hata wanafunzi hivyo kushindwa kufanya vizuri.

“…Mitaala imevurugwa sana, kunamchanganyiko wa masomo nadhani unakumbuka kuna kipindi baadhi ya masomo yaliunganishwa kama Jiografia, Historia na Uraia wakaita maarifa ya jamii…kipindi hiki wanafunzi walifanya vibaya sana hivyo ikabadilishwa sasa watoto wanafanya vizuri tofauti na awali,” alisema Karigita.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Lwengera Darajani, Youze Mbwambo alisema idadi kubwa ya masomo kwa wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la tatu ni chanzo kingine cha wanafunzi hao kufanya vibaya kwani wamekuwa wakibebeshwa mzigo pasipo sababu za msingi.

Akizungumzia hoja hizo zilizotolewa na baadhi ya walimu, Ofisa Elimu Taaluma, Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Elius Mkwizu alisema mabadiliko yanayofanywa na wataalamu hufanywa kwa malengo mazuri licha ya kuwepo na changamoto kadhaa maeneo tofauti.

*Habari hii imeandaliwa na Mtandao wa Thehabari.com (www.thehabari.com) kwa kushirikiana na Taasisi ya HakiElimu.

Wednesday, August 15, 2012

Maoni ya wadau wa Elimu kuhusu Bajeti ya Elimu haya hapa. Kiswahili na Kingereza




Maoni ya Wadau wa Elimu kuhusu Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iliosomwa Bungeni 13 Agosti, 2012 - HakiElimu, Dar es Salaam.
HakiElimu inalitazama suala la elimu kwa kila mtu kama haki ya msingi baada ya haki ya kuishi, kwetu sisi elimu ndiyo haki pekee inayoweza kumsaidia mtoto au mwanadamu yoyote aweze kupata haki zake nyingine zote. Kwa sababu hiyo, HakiElimu inaamini kuwa suala la kupambana na changamoto zinazoikabili sekta ya elimu nchini si la kufumbiwa macho na ni jukumu la kila Mtanzania. 

Kama shirika linalojihusisha na utetezi wa haki ya kupata elimu, HakiElimu iliandaa na kufanya mkutano na wadau wa elimu mbalimbali uliyolenga kujadili hali ya elimu nchini, kufuatilia Bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya 2012/2013, ikiwasilishwa Bungeni  tarehe 13 Agosti, 2012 na kutoa maoni, mitazamo na ushauri juu ya bajeti hiyo na mwelekeo wa elimu kwa ujumla.

1.      Katika hotuba yake Waziri hajazungumzia kabisa mgomo wa walimu uliofanyika hivi karibuni. Hii inatia shaka kama serikali ina nia ya dhati kushughulikia kero na matatizo ya walimu. Kama serikali inataka kufikia muafaka na walimu na kuboresha ufundishaji ni lazima ikubali kuwa kuna tatizo na isikwepe wala kuona aibu kulijadili suala hili kwa uwazi. Aidha, Bajeti haina mkakati maalumu wa kuongeza ubora wa walimu ambao ni muhimu katika kuleta elimu bora. Serikali imeendelea kupuuza maslahi ya walimu huku ikikataa kukubali kuwa bila kukuboresha maslahi yao hawatafanya kazi kwa moyo.
 
2.      Waziri pia hakugusia vizuri suala la migomo ya wanafunzi vyuo vikuu ambayo mingi husababishwa na matatizo ya Bodi ya Mikopo. Ni muhimu kubadilisha mfumo wa utoaji wa mikopo; Bodi ya Mikopo iwe na matawi mikoani ili kurahisisha utoaji wa mikopo na kupunguza urasimu. Pia, katika kupunguza kero zilizopo kwa wanafunzi wasiokuwa na uwezo wa kujilipia masomo ya juu, Serikali ingekuja na mkakati wa kuwasomesha wanafunzi waliofaulu kwa kiwango cha juu. Hii ingekuwa tumaini kwa watoto wanaotoka kwenye familia masikini.

3.      Bajeti hii haina tofauti yoyote na ile ya mwaka jana kwa maana ya uwezo wa kutatua changamoto za elimu na hatutegemei mapya katika utekelezekaji wake. Bajeti haizungumzii kwa kina jinsi ya kukabiliana na changamoto zilizopo katika sekta ya elimu; haina upembuzi yakinifu wa matatizo na njia za kuyatatua. 

4.      Bajeti bado inatoa kipaumbele katika matumizi ya kawaida na kupuuza uwekezaji wa msingi katika elimu. Mathalani, katika makadirio ya bajeti ya takribani shilingi bilioni 724, ni shilingi bilioni 92.5 tu zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo katika elimu. Hii ina maana kuwa ni asilimia 13 ya bajeti itaenda kwenye shugghuli za maendeleo na zaidi ya bilioni 630 (87%) zimekwenda katika matumizi ya kawaida!
5.      Aidha, suala lingine lililojitokeza ni utegemezi mkubwa wa Serikali kwa fedha za wahisani katika kutekeleza miradi yake ya maendeleo. Katika Bajeti hii kati ya shilingi bilioni 92.5 zilizotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, ni shilingi bilioni 18.5 (asilimia 20) tu ndizo zitatoka katika vyanzo vya ndani wakati shilingi bilioni 74 (asilimia 80) zinatarajiwa kutoka kwa wahisani! Utegemezi kwa wahisani wa kiwango kikubwa hivi ni hatari kwa maendeleo ya nchi yetu kwani kama wahisani hao watakwama kutoa misaada yao basi mipango yetu ya maendeleo  nayo itakwama 



6.    Tumemsikia Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi akisema uwiano wa mwalimu kwa wanafunzi umeboreshwa kutoka 1 kwa 48 hadi 1 kwa 46. Kwa juu juu, inaonekana tumefanya vizuri, kwani lengo letu ni kufikia uwiano wa 1 kwa 45. Lakini kuna angalizo; huu ni wastani na unaficha ukweli kwamba katika maeneo mengi watoto wanaweza kuzidi 50, 60 au 70 kwa mwalimu mmoja. Bajeti ikijaa maelezo yanayojikita kwenye kutoa wastani bila ufananuzi kuhusu hali halisi ni hatari sana kwani haitoi taswira halisi ya ama kukua,  kudumaa au hata kudorora kwa elimu nchini.
7.      Waziri ameahidi kwamba katika kipindi cha 2012/13, Wizara yake itaifanyia kazi sera mpya ya elimu; lakini, hajasema ni lini sera hiyo itakuwa tayari. Tunasistiza umuhimu wa kutimiza ahadi hii mapema kwani sera hii ndiyo itaongoza utoaji wa elimu Tanzania. Sera ya 1995 imepitwa na wakati na sasa ni serikali inapaswa  ije na sera mpya inayozingatia mabadiliko ya kiuchumi na dira ya maendeleo.
8.      Serikali imeendelea kutoa ahadi juu ya mpango mpya wa maendeleo ya elimu ya msingi awamu ya tatu baada ya ule wa awamu ya pili kumalizika 2010, lakini haielezi maandalizi yamefikia hatua gani na lini utakuwa tayari. Ni vema serikali ikaharakisha mpango huo ili kutoa dira kwa watekelezaji wa sera na bajeti za kila mwaka.
9.      Hotuba ya Waziri imeendelea kupuuza matatizo katika shule za kata hasa suala la kutokuwa na mabweni. Kuna athari nyingi sana za kuwa na shule umbali mkubwa kutoka makazi ya wanafunzi. Hii ni pamoja na wasichana kuwa hatarini kupata mimba n.k. Serikali haijasema wala kuonesha mkakati madhubuti wa kuyafanyia kazi matatizo kama haya.
10.  Alipokuwa akiongelea suala la ubora, Waziri alijikita zaidi katika kuongelea namna Wizara ilivyoboresha matokeo katika mtihani wa kuhitimu shule ya msingi, kutoka asilimia 53.5 hadi 58.3. Wakati kweli hili ni ongezeko, bado haliridhishi. Aidha, kumekuwa kuna tatizo kubwa sana kwenye ufaulu wa mtihani wa kuhitimu kidato cha nne kwani asilimia 90 ya waliofanya mtihani huu mwaka jana walipata div 4 au 0. Utoaji wa elimu bora ya sekondari utaisadia sana Tanzania kufikia malengo yake ya maendeleo kwani mwananchi anayeipata atakuwa na uwezo mkubwa wa kulinda afya yake, kujiendeleza kiuchumi na kujitambua. Hivyo, tunashangazwa na kushtushwa na ukimya wa Waziri kuhusu suala hili.
11.  Wakati tunatarajia kuandaa sera mpya ya elimu ni vema pia tukatafakari kuhusu suala la lugha ya kufundishia. Wakati ni muhimu kwa Mtanzania wa karne hii kukijua Kiingereza na ufundishaji wa lugha hii lazima uboreshwe, ni muhimu zaidi kuwafundisha watoto kwa lugha ambayo wanaielewa ili wapate ujuzi.
12.  Mwisho, wakati Wizara inapanga mikakati yake, ni muhimu kuwa na mpango madhubuti kuhusu wahitimu kwani kundi hili likikata tamaa kutokana na kushindwa kupata ajira n.k., linaweza kuleta mtikisiko mkubwa katika taifa.




Education stakeholders’ response to the Ministry of Education and Vocational Training budget reading on 13th August 2012 – HakiElimu, Dar es Salaam.
HakiElimu’s vision is to see an open, just and democratic Tanzania, where all people enjoy the right to education that promotes equity, creativity and critical thinking. We believe that for this to happen, people need to be involved in shaping the country’s public education system at all levels.
This is why on August 13, 2012, HakiElimu brought together various stakeholders to discuss the state of education, listen to the reading of the Ministry of Education and Vocational Training 2012/2013 budget and discuss how effectively it addressed their varying concerns. The meeting was held on the premises of REPOA in Dar es Salaam and culminated in the following recommendations and concerns:
1.      It was surprising that the Minister made no mention of the teacher’s strike. For many around the country, this was one of the most significant events in the education sector this year. By not speaking about it, the Ministry and Government gave the public the impression that they are not interested in improving teachers’ welfare. If the Ministry hopes to improve learner outcomes, it must be open and transparent in dealing with teachers’ concerns and these must be prioritised in the quest for quality education.


2.      The minister’s budget speech failed to highlight enduring strikes by students in higher learning institutions as a challenge. These strikes are most often caused by students’ dissatisfaction with the higher learning loans system and might be significantly reduced if the system was decentralized so that the Loans Board worked through offices at regional level. Government should introduce a scholarship system so that students who distinguish themselves through their performance are assured that their studies will be paid for.  This avenue would provide hope to students from poor families.
3.      This budget is no different than last year’s budget in terms of how it will address current challenges in the education sector; we don’t expect anything new as a result of its implementation. The budget does not discuss at length strategies that will be used to address education sector challenges, it does not critically analyse underlining issues and concerns.
4.      This year’s budget continues to privilege recurrent over development expenditures thus neglecting the opportunity, yet again, to invest in education. Out of an estimated expenditure of approximately 724 billion shillings, just 92.5 billion has been budgeted for development efforts. In contrast, over 630 billion shillings has been allocated for recurrent expenditures.
5.      Another issue that emerged had to do with the Ministry’s dependency on funds from development partners in order to implement development projects. In this year’s budget, out of the 92.5 billion shillings allocated to development projects, just 18.5 billion or 20 per cent will be generated from internal or local revenue sources. The rest, which is 74 billion shillings or 80 per cent of the development budget, is expected to be financed by development partners. This level of dependency on external sources is worrying given  that development partners sometimes renege on commitments to make funds available.


6.      In his speech the Minister of Education and Vocational Training mentioned the improvement in teacher-pupil ratio, from 1 to 48 to 1 to 46. On the surface, it would appear we have done well in this area, given that our objective is to have at least 1 teacher to 45 pupils. But in reality, the figure given is an average and across the country there are classrooms with over 50, 60 and even 70 pupils to one teacher. The use of averages in presentations such as this one without further explanation is misleading and consequently fails to provide the public with a real picture of what is going on in education.
7.      The Ministry expects to finalise the new education policy document during this financial year, although it has not said specifically when. We would like to urge the Ministry to make sure that this happens because the 1995 education and training policy is out of date. It is important that the government finally releases a new policy that takes into account changes in the economic context and development vision of the country.
8.      The Government, through the Ministry of Education and Vocational Training, committed itself to implementing a third phase of the primary education development programme, after the second phase came to an end in 2010. We urge the Government to ensure that this programme is ready for implementation and that it carries a vision for the positive transformation of primary education in Tanzania.
9.      The budget speech continued in the tradition of underestimating the challenges that community secondary schools are facing, and particularly the lack of hostels at these schools. There are several cons to having schools located at a long distance from where learners and their communities live; it is particularly dangerous for girls and increases the incidence of schoolgirl pregnancies and other undesirable situations. The Ministry failed to clearly explain how it will work to address challenges such as these in the coming financial year.
10.  When discussing the issue of education quality, the Minister focused on how the Ministry had successfully raised the primary school pass rate from 53.5 to 58.3 per cent. While this is indeed an improvement, it is still not satisfactory and more needs to be done to improve learner outcomes. This is particularly urgent at secondary school level, where in the most recent form four exams, 90 per cent of the examination candidates record a dismal performance of division four or zero. The provision of quality secondary education is fundamental to the development of this country because of its potential impact on human development and particularly in the areas of health and citizen agency. We are shocked and surprised that the Minister failed to mention this.
11.  While the Ministry undertakes to finalise and release a new education policy, it is important that the issue of language of instruction is finally addressed. While it is important for Tanzania’s to become competent users of the English language, and teaching of this language in our schools must improve, our priority should lie in ensuring that learners are taught in a language that they understand and that can impart them with the skills they need.
12.  Finally, as the Ministry develops its plans and strategies, it is important that it comes up with a strategy for addressing the high levels of youth unemployment as if the current situation  continues unchecked, it could lead to civil disturbance and unrest.





Msingi dhaifu madarasa ya awali chanzo cha wasiojua kusoma, kuandika

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Silabu Mizeki Charahani (kulia) akimtembeza mwandishi wa Thehabari.com (hayupo pichani) kuangalia mazingira ya shule hiyo alipotembelea shule hiyo. Silabu ni moja ya shule zisozokuwa na madarasa ya awali Wilaya ya Korogwe.

Mhariri Mkuu wa Thehabari.com, Joachim Mushi (kushoto) akifanya mahojiano
 na baadhi ya wakazi wa Lwengera Darajani wilayani Korogwe

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Lwengera Darajani, Youze Mbwambo akionesha
 jengo ambalo ni nyumba ya mwalimu ambayo inatumika kwa muda kama darasa la awali.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Lwengera Darajani, Youze Mbwambo akizungumza
 na mwandishi wa Thehabari.com Korogwe, Tanga. Shule hii haina darasa la awali.

Baadhi ya shule za msingi ndio kwanza zinajenga madarasa ya awali. Hili ni darasa la awali la shule ya msingi Kitopeni Korogwe

MSINGI mbovu na dhaifu wa elimu kwa madarasa ya awali umebainika kuwa chanzo cha baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi mkoani Kilimanjaro na Tanga kumaliza elimu hiyo huku hawajui kusoma na kuandika.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi hivi karibuni katika Wilaya ya Moshi (Manispaa) umebaini idadi kubwa ya shule za msingi awali hazikuwa na madarasa ya awali kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi kujiunga na darasa la kwanza, jambo ambalo liliilazimu shule kupokea wanafunzi wa darasa la kwanza toka nje ya shule wengine wakiwa hawajaandaliwa kikamilifu.

Taarifa zimebaini vituo vingi vya shule za awali ambavyo baadhi ya shule za msingi zilikuwa zikitegemea kupokea watoto wa darasa la kwanza vilikuwa havina walimu wenye taaluma ya kuwaandaa watoto katika vituo hivyo kwa ajili ya kujiunga na darasa la kwanza.
Uchunguzi uliofanyika katika baadhi ya shule za katikati ya Mji wa Moshi (Manispaa) na pembezoni umebaini shule nyingi hivi sasa zimeanzisha madarasa ya awali ikiwa ni shinikizo la Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi la miaka ya hivi karibuni.

Shule ya Msingi Magereza ni miongoni mwa shule zinazofanya vibaya katika Manispaa ya Moshi, shule hii inashika nafasi ya 45 kiwilaya kati ya shule 46 za manispaa nzima. Kimkoa inashika nafasi ya 595 kati ya shule 638 japo ipo mjini ukilinganisha na zile za vijijini.
Akizungumza mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Magereza alisema awali haikuwa na darasa la awali bali ilikuwa ikipokea wanafunzi wa darasa la kwanza kutoka nje ya shule. Alisema ilianzisha darasa la awali rasmi linaloendeshwa na shule hiyo Machi 1, 2012.

Taarifa zaidi zimebaini licha ya madarasa mengi ya shule za awali kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi ambao huwa mzigo kwa mwalimu mmoja anayefundisha, mengi ya madarasa hayo yana umri kati ya miaka mitatu kushuka chini jambo ambalo linaonesha mafanikio yake hayajaanza kujitokeza.
Hata hivyo hali hiyo imejitokeza katika Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, kwani kati ya shule nne za msingi Silabu, Lwengera, Kitopeni na Boma ambazo mwandishi amezitembelea ni moja tu (Boma) ndio yenye darasa maalumu la wanafunzi wa awali. Uchunguzi umebaini kuwepo na shule zenye wanafunzi wa awali lakini hakuna vyumba vya kufundishia wala waalimu wenye sifa ya kufundisha kitengo hicho muhimu.

Akizungumza Ofisa Elimu Taaluma, Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Elius Mkwizu alisema kwa eneo lao bado suala la vyumba vya madarasa ni tatizo hivyo idara hiyo inajitahidi kulishughulikia suala hilo kwa kushirikiana na wazazi wa maeneo husika.
Kwa upande wake Kaimu Ofisa Elimu Manispaa, Leocadia Akaro alisema idara yao inajitahidi kuhimiza ujenzi wa madarasa ya awali na mafanikio ni makubwa kwani idadi kubwa ya shule za msingi zinamadarasa ya awali tofauti na ilivyokuwa hapo nyuma.
Habari hii imeandaliwa na Mtandao wa Thehabari.com (www.thehabari.com) na taasisi ya HakiElimu

Tuesday, August 14, 2012

HakiElimu, Wasomi UDSM waikosoa bajeti ya elimu ‘live’

Kutoka kushoto ni Meneja Kitengo cha Habari wa HakiElimu, Nyanda Shuli, 
Mhadhiri Adolf Mkenda kutoka Idara ya Uchumi ya UDSM 
Mhadhiri wa UDSM, Dk. Kitila Mkumbo
Mhadhiri mwenzao kutoka Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano, Ayoub Rioba
 akizungumza katika mjadala huo.
Wahudhuriaji wakiangalia Bunge wakati Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi 
Dr Shukuru Kawambwa akiwasilisha mapato na matumizi ya wizara yake 
kwa mwaka wa fedha 2012/2013.Bajeti ya wizara hiyo inategemewa kupitishwa Leo


Baadhi ya maofisa kutoka taasisi ya HakiElimu wakifuatilia mjadala huo

TAASISI ya HakiElimu leo jijini Dar es Salaam imewakutanisha baadhi ya wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), walimu pamoja na wadau mbalimbali wa elimu ambapo waliishuhudia bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Elimu ikiwasilishwa ‘live’ mjini bungeni mjini Dodoma kabla ya kutoa maoni yao.

Wadau hao wa elimu kwa pamoja waliishuhudia kupitia king’amuzi bajeti ya Wizara ta Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikiwasilishwa ‘live’ wakiwa kwenye mkutano kisha baadaye kutoa maoni yao jijini Dar es Salaam.
Akizungumza mara baada ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Elimu, Dk. Shukuru Kawambwa kuwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2012/13, Mhadhiri wa UDSM, Dk. Kitila Mkumbo alisema ameshangaa bajeti hiyo kutouona mgomo wa walimu wa juzi pamoja na migomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu kama ni tatizo kwa elimu na kuiingiza kama changamoto.

“Binafsi kati ya vitu ambavyo vimenishangaza ni bajeti hiyo kutotaja mgomo wa walimu katika bajeti iliyopita kuwa ni miongoni mwa changamoto za wizara hiyo…na hata migomo ya vyuo vikuu,” alisema Dk. Mkumbo alipokuwa akijadili katika mkutano huo.

Mhadhiri wa UDSM, Dk. Kitila Mkumbo akiwasilisha mada kabla ya mjadala huo
 Alisema wizara imetaja kufanya vizuri katika elimu upande wa msingi na sekondari kwa kidato, lakini imekwepa kutoa mafanikio kwa kidato cha tano na sita eneo ambalo limefanya vibaya kwa matokeo ya hivi karibuni. Alikosoa kiwango cha uwiano kati ya wanafunzi na walimu kilichotatolewa kwa sasa (1:46) kwani idadi kubwa ya walimu wapo shule za mjini huku hali mbaya ikiwa vijijini.
Aidha aliongeza kuwa wizara pia imeshindwa kuona migomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu ya mara kwa mara ni changamoto hivyo kushindwa kueleza katika bajeti yake. “…karibu asilimia 80 ya migomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu imesababishwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, lakini hili halikutajwa katika bajeti ya waziri,” alisema msomi huyo.
Kwa upande wake Mhadhiri Adolf Mkenda kutoka Idara ya Uchumi ya UDSM akizungumza katika mkutano huo alisema bajeti iliyowasilishwa ni ya kawaida hivyo ni vigumu kumaliza changamoto lukuki za elimu zinazoikabili wizara hiyo.
 
Umati wa wasomi waliojumuika katika warsha hiyo ya kuijadiri bajeti ya 
Elimu na Mafunzo ya Ufundi


Alisema bajeti imejivunia ongezeko la idadi ya vyuo vikuu lakini imeshindwa kuonesha ubora wa vyuo hivyo jambo ambalo ni hatari endapo litaachwa, bila udhibiti. “…Twaweza kuwa na vyuo vingi lakini suala la ubora ni tatizo lingine. Pia uandikishaji wa idadi kubwa ya wanafunzi unatakiwa kulinganishwa na waliokusudiwa kuandikishwa…maana twaweza jivunia kiwango kinapanda kumbe tunadanganywa na ongezeko la idadi ya watu,” alisema msomi huyo.

Akizungumza kwenye mjadala, Kaimu Mkurugenzi  wa HakiElimu, Nyanda Shuli alisema Serikali haiwezi kufanikisha elimu bora bila kuaandaa walimu bora katika utoaji wa elimu husika. “Huwezi kutegemea elimu bora pasipo na walimu bora, binafsi sijaona mkakati wowote mahususi wa kuboresha elimu,” alisema Shuli.
Ameishauri wizara ya elimu kujiandaa vizuri kimipango kabla ya kutekeleza mpango wa kuwa na shule ya kidato cha tano na sita kwa kila tarafa ili kuepuka madudu yaliojitokeza katika mpango wa uanzishwaji shule za kata.
Hata hivyo kabla ya kuishuhudia bajeti hiyo ikiwasilishwa Dk. Mkumbo na Mkenda wakiongozwa na mhadhiri mwenzao kutoka Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano, Ayoub Rioba waliwasilisha mada zilizokuwa zikiiangalia elimu ya Tanzania na majaliwa yake.

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Elimu tayari imewasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2012/13 ambapo jumla ya sh. 724,471,937,000 ili zitumike kuiwezesha Wizara kutekeleza majukumu yake. Huku sh. 18,561,689,000 zikiwa ni fedha za ndani na sh. 74,019,627,000 kutoka kwa washirika wa maendeleo.

Habari na HakiElimu kwa kushirikiana na TheHabari.com


Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More