Wednesday, October 10, 2012

Ben Pol aonesha kuwa msanii ni kioo cha jamii


Ben Pol msanii wa bongo flavor na mshindi wa tuzo za muziki za Kilimanjaro 
kwa mwaka 2011 na 2012 akiwa na bango la 'Boresha Chekchea'.

 Ule usemi wa kuwa msanii ni kioo cha jamii unajidhirisha kwa msanii wa mziki wa bongo flavor Bernard Michael Paul Mnyang'anga anae julikana kisanii kama Ben Pol kuunga mkono kampeni ya kuboresha elimu ya awali Tanzania.

Kampeni hiyo ilizinduliwa na HakiElimu tar 27 September 2012 iliyoambatana na uzinduzi wa matangazo mawili ya Television na redio kwaajili ya kuendeleza kampeni hii ya elimu ya awali iliyopewa jina la Chekechea.Matangazo hayo yanaonesha changamoto zilizoko katika elimu ya awali nchini na kutoa mfano wa shule bora au elimu ya awali inayotakiwa nchini Tanzania
 
Ben Pol akiwa katika baadhi ya kazi zake za kisanii jukwaani

 
Elimu ya Awali ni muhimu kwa maendeleo ya mtoto kimwili, kiakili na kimaadili. Katika Sera ya Elimu na mafunzo ya mwaka 1995 Serikali inaonesha umuhimu wa elimu ya awali,inapotamka ; “Tafiti kadhaa zilizofanyika nchini katika miaka ya 1980 zilibaini kuwa watoto waliopitia elimu ya awali huwa na mafanikio makubwa zaidi wanapoanza darasa la kwanza. Kutokana na kutambua umuhimu huu, Serikali iliamua kuingiza Elimu ya Awali kwa watoto wenye umri wa miaka 5 na 6 kwenye mfumo rasmi wa elimu na kila shule ya msingi inapaswa kuwa na madarasa ya Elimu ya Awali.”
Sera ya Elimu na Mafunzo 2010. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi . Toleo jipya Rasimu ya 2 March 2011.(uk 5-6).

Uwekezaji katika huduma bora kwa mtoto na elimu ya awali huwa na faida maradufu kwa watoto wetu- ambao ni raia wetu wa  baadaye. Walipa kodi nao pia hufaidika na huimarisha uchumi. Faida ya uwekezaji wa fedha za umma katika elimu bora ya awali ni kubwa sana. Lakini je, Tanzania imeligundua hili na kulitekeleza kikamilifu?  Na je, maneno haya ambayo sera inasisitiza yako yanatekelezwa kwa vitendo?



0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More