Wednesday, June 13, 2012

Uhaba wa madawati bado ni changamoto shule za msingi Musoma

Wanafunzi wa shule ya Msingi Etaro wakiwa darasani wakimfuatilia mwalimu.wanafunzi wengi katika shule hii wanakaa chini kutokana na uhaba wa madawati.

Wanafunzi wakiendelea na masomo yao huku wengine wakitumia magoti yao kama sehemu za kuandikia huku wakiwa wamekaa chini.

Uhaba wa madawati katika shule za msingi na sekondari umeendelea kuumiza vichwa vya wapenda elimu pamoja na wazazi kwa ujumla nchini.

Upungufu wa madawati katika shule za msingi umeendelea kudidimiza kiwango cha elimu nchini huku ukichangia kuongezeka kwa utoro kwa kusababisha wanafunzi wengine kukata tamaa ya kusoma na mazingira ya shule kwa ujumla ambayo si rafiki kwao.

Matokeo ya wanafunzi kukaa chini husababisha wanafunzi kuandika wakiwa wameinama na wengine hata kulala kifudi fudi na wengine kuchuchumaa na hivyo kushindwa kuandika vizuri na pia kuchoka mapema.Hali hii kupelekea matokeo mabaya nyakati za mitihani hasa ya kitaifa.


Hali halisi ndiyo hii wilayani Musoma vijijini


Wanafunzi wengine wakiyageuza madawati mabovu angalau wapate sehemu ya kukaa

Wengine wanatumia viatu vyao kukalia, na wasio na viatu wanakaa kwenye vumbi


0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More