Friday, June 1, 2012

Tazama kipindi cha Tafakari Time kupitia ITV leo saa moja kamili jioni kuhusu maisha ya geto kwa wanafunzi

Ongezeko la shule za sekondari za kata limeleta maisha mapya kwa wanafunzi wanaosoma shule hizo.Wanafunzi wengi wanatoka mbali na shule zilipo na hivyo kuishia kupanga vyumba mtaani katika vikundi na kuishi waisha ya kuchangia kila kitu (maisha ya geto).

Maisha ya geto kwa wanafunzi ni njia mbadala ambayo wanafunzi wanatumia ili kukabiliana na uhaba wa mabweni mashuleni hasa shule za kata, maisha haya ya geto yameelezwa kuwa ni chanzo cha kufanya vibaya kwenye mitihani ya taifa, kuzuka kwa tabia mbaya kwa wanafunzi kama uvutaji wa bangi, ngono nzembe zinazopelekea wanafunzi wengi hasa wa kike kuishia kupata mimba.

Fuatana nasi katika mfululizo wa vipindi utakao kufungua macho wewe mzazi, mlezi na serikali juu ya maisha halisi ya watoto wetu huko mashuleni.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More