Tuesday, April 24, 2012

Uzinduzi wa shindano la Insha na Michoro la HakiElimu katika picha



Mwenyekiti wa jukwaa la katiba, Deus Kibamba akitoa ufafanuzi wa shindano la Insha na michoro lenye kichwa cha habari 'Katiba mpya iseme nini kuhusu elimu?' nia ya shindano hili ni kutafuta mawazo ya watanzania wa kada zote juu ya mchakato wa uandikaji katiba mpya na elimu isemweje ndani ya katiba?


Meneja katika idara ya habari na utetezi, Nyanda Shuli akifafanua malengo ya insha na mategemeo ya HakiElimu.Pia alitangaza zawadi kwa washindi watakaopatikana.Hata hivyo ndugu Shuli aliweka sawa kuwa watakaotangazwa mwisho wa shindano ni washindi tuu na si vinginevyo.


Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini maelezo toka kwa watoa maada wa HakiElimu na Jukwaa la katiba huku wakichukua matukio kwaajili ya kuwapasha watanzania.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More